Kuhusu Sisi

IA Watch, ikiwa ni sehemu ya Chuo cha Chanjo, ni tovuti yenye video fupi za kujifunza kwa haraka ujuzi muhimu wa chanjo kupitia simu au kompyuta yako.
IA Watch inakuruhusu:
  • Tazama Video Mtandaoni au nje ya Mtandao
  • Fuatilia maendeleo ya kujifunza kwako
  • Unda orodha ya video zako upendazo au ulizotazama kwa wingi
  • Jipatie alama na sifa za kitaalamu

Unaweza kuingiza IA Watch kwenye kazi yako kwa njia nyingi, ikiwemo:

  • Kuboresha na kuamsha upya ujuzi wako
  • Kama rejea rahisi wakati wa kufanya majukumu ya msingi
  • Kusaidia mawasiliano na wafanyakazi wengine
  • Kuimarisha Usimamizi Saidizi
Maudhui ya Kuaminika

Video zote zinatokana na mwongozo uliothibitishwa wa WHO na umetengenezwa kwa msaada wa bodi ya ushauri ya afya iliyo na wataalam wa kimataifa na watendaji wa ndani wa maeneo husika.

Video zote zinapatikana kwa Kiingereza, Kifaransa na Kiswahili na Hausa, na lugha zingine kuongezwa hivi karibuni.

Mchakato wa Uhariri

Kama sehemu ya ubunifu unaojali mahitaji ya watumiaji, Taasisi ya BCL ilifanya ve research to identify the current challenges and content priorities of the target audience and key stakeholders.

Mahojiano ya kina, mahojiano ya vikundi, na vipindi ya kufanya kazi na makundi ya watumiaji Tanzania. Kulingana na na haya na miongozo ya chanjo iliyopo ambayo imewekwa na WHO, orodha ya mada zenye umuhimu za video zilianzishwa na kupitishwa na walengwa.

Baada ya kuthibitishwa, kila mada ya video ilitafitiwa kwa kutumia mwongozo wa WHO na mahoiano na wataalam wa mada husika. Video zilipitiwa na kuboreshwa na jopo la wataalam wa mada husika, pamoja na wadau kutoka Wizara ya Afya Tanzania. Mchakato wa uhariri na mapitio ulifanywa kwa uhuru, bila kuwa na kuingiliwa kokote zaidi ya kule kulikolezewa hapo juu.

Bodi ya Ushauri

Watu wafuatao wamepitia nyaraka za mafunzo na kutoa mwongozo kuhusu mada za mafunzo ya chanjo.

  • Dr. Francois Gasse, UNICEF
  • Dr. Renu Paruthi, Ofisi ya WHO nchini India
  • Bonaventura Nestory, Daktari, kutoka Wizara ya Afya Tanzania
  • Jean-Marc Olive, Daktari, mwanachama wa WHO IPAC (Immunization Practice Advisory Committee), amestaafu kutoka WHO
  • Frida Mghamba, Wizara ya Afya Tanzania (zamani) Daktari
  • David Brown, Brown Consulting Group
  • Alex Mphuru, Daktari, Wizara ya Afya Tanzania (zamani)
  • Robin J. Biellik, PATH (amestaafu) na WHO (amestaafu)
Wadhamini wetu

Immunization Academy ni mpango wa mafunzo duniani kote unaoongozwa na wataalam wa mafunzo wa Taasisi ya BCL Institute. Mpango huu unadhaminiwa na msaada kutoka kwa mfuko wa Bill na Melinda Gates na umeundwa kwa kutumia mwongozo uliothibitishwa na WHO, ukijumuisha mafunzo kwa mameneja wa ngazi ya kati(MLM) na Chanjo Kivitendo (IIP).

Wasiliana nasi
[email protected]